Maelezo ya jumla

Taasisi ya Ruhi hufanya kozi na programu za kielimu kwa makundi ya umri anuai, kutoka umri mdogo wa 5 au 6 hadi utu uzima. Yaliyotolewa hapo chini ni maelezo ya jitihada zake tatu za hivi karibuni, pamoja na orodha ya nyenzo zinazotumika kwa kila moja. Lazima ieleweke kwamba orodhoa zitaendelea kupata mabadiliko kadri tajiriba ugani inapokua, na majina mapya yataongezwa kadri idadi ya vipengele vya kimtaala vinavyoendelea kukuzwa vifikiapo hatua ambapo vinaweza kusambazwa kwa upana.

Mlolongo mkuu wa kozi, kwa ajili ya wale wenye umri wa miaka 15 na watu wazima

Hapo chini yapo majina ya vitabu vilivyopo kwa sasa katika mlolongo ulioandaliwa na Taasisi ya Ruhi kwa vijana na watu wazima. Vitabu hivi vinakusudiwa kutumika kama mlolongo mkuu wa kozi katika juhudi ya hatua kwa hatua ya kuongeza uwezo wa vijana na watu wazima kuhudumia jumuiya zao. Taasisi ya Ruhi pia ina  kuza seti ya kozi zinazochepuka kutoka kitabu cha tatu katika mlolongo kwa ajili ya kuwafunza walimu wa madarasa ya watoto ya Kibahá’í, hali kadhalika seti nyingine kutoka kitabu cha tano kwa ajili ya kuinua wahuishaji wa vikundi vya vijana chipukizi. Hizi, pia, zimeoneshwa katika orodha hapo chini.

Programu ya uwezeshwaji kiroho wa vijana chipukizi

Tangu kuanzishwa kwake, taasisi ya Ruhiimeweka umuhimu maalum kwenye kazi yake na vijana wenye umri wa miaka 12 hadi 15, hasa, imetafuta kuelewa mienendo ya kudumisha vikundi vidogo katika jumuiya za mahali ambavyo hutoa eneo ambapo vijana wanaweza kujadili mawazo na kuunda utambulisho imara wa kimaadili. Taasisi imegundua majina yaliyoainishwa hapo chini kwa ajili ya kusudi hili. Yamegawanyika katika makundi mawili na yameorodheshwa katika mpangilio wa ugumu.Majina mengine kadhaa hatimaye yataongezwa kwenye programu ya Taasisi kwa ajili ya uwezeshwaji kiroho wa vijana chipukizi.

Majina yote haya yanahusika na maendeleo ya ujuzi wa lugha na nguvu ya kujieleza.Baadhi katika kundi la kwanza pia huelezea dhana za kihisabati na masuala ya kijamii, wakati mengine hutafuta kuandaa vijana kuuendea uchunguzi wa uhalisia wa kimwili, kijamii na kiroho katika namna ya kisayansi. Ingawa dhana za kiroho katika zana za kundi la kwanza zimechotwa kutoka mafundisho ya Kibahá’í, kwa asili siyo za kidini, wala hazishughulikii mada ambazo hasa ni za Kibahá’í. Aina nyingi za mashirika, ikijumuisha taasisi za kielimu, kwa hiyo zitagundua kuwa za kufaa kwa ajili ya programu zao za kielimu kwa vijana chipukizi. Majina ya sasa katika kundi hili ni:

Pepo Nyanana za Uthibitisho
Chemchemi ya Furaha
Tabia za Akili Yenye Mpangilio
Dalili za Matumaini
Kutembea Njia Nyoofu
Juu ya Afya na Ustawi
Kujifunza Kuhusu Ubora
Kufikiri Kuhusu Nambari
Uchunguzi na Umaizi
Hekalu la Binadamu
Kuchota kutoka Nguvu ya Neno

Katika kazi yake yenyewe na vijana, Taasisi ya Ruhi hujumuisha vitu katika kundi la pili, ambalo huwasilisha mada za Kibaha’i. Miongoni mwa mada hizi ni zile ambazo vijana wengi chipukizi mara nyingi husumbuka nazo kama vile, hiari na masaibu na uhusiano tata kati ya hiari na ustadi. Kwa sasa, majina yafuatayo yapo katika kundi hili:

Roho ya Imani
Nguvu ya Roho Mtakatifu
Miale ya Mwangaza

Programu ya uwezeshwaji kiroho inatolewa kwa vijana chipukizi katika makundi madogo, mara nyingi huundwa katika kijiji au ujirani na kijana mkubwa. Taasisi ya Ruhi inaendeleza mlolongo wa kozi za mchepuo, kwa kuanza na Kitabu cha 5 katika mlolongo wake mkuu, kuandaa vijana wakubwa na watu wazima kuhudumia kama “mhuishaji”wa vikundi hivyo. Kama unavutiwa katika kusoma maoni kutoka wale ambao wamekwisha shiriki katika programu, bonyeza hapa.

Madarasa ya Kibahá’í ya watoto kwa ajili ya elimu ya kiroho

Masomo kwa ajili ya madarasa ya Kibahá'í ya watoto,yakianza na Daraja la 1 kwa ajili ya umri wa miaka 5 au 6, yamewasilishwa katika muktadha mafunzo ya mwalimu. Wakati watu kila mahali wana hamu ya watoto wao kushiriki kwenye madarasa kwa ajili ya elimu yao ya kiroho, tajiriba imeonesha kuwa changamoto imejikita kwenye ufunzaji wa idadi ya kutosha ya walimu kukidhi hitaji hili. Taasisi ya Ruhi inaendeleza seti ya kozi kwa ajili ya mafunzo ya walimu wa madarasa ya Kibahá'í ya watoto ambayo imejitokeza kutoka kitabu cha tatu katika mlolonfo mkuu, na zana zinazohitajika kwa ajili ya madarasa yenyewe yatawasilishwa katika kila kitabu. Hasa wakati wa miaka ya mwanzoni ya utoto, msisitizo mkubwa umewekwa kwenye maendeleo ya sifa za kiroho na kwenye zile imani, tabia na mitindo ya mwenendo ambayo imejumuisha sifa za lazima za kiumbe wa kiroho.

Kufundisha Madarasa ya Watoto, Daraja la 1
Kufundisha Madarasa ya Watoto, Daraja la 2 (toleo la kabla ya uchapishaji)
Kufundisha Madarasa ya Watoto, Daraja la 3 (toleo la kabla ya uchapishaji)
Kufundisha Madarasa ya Watoto, Daraja la 4 (zana inayoendelezwa)

Zana zilizojumuishwa hapo juu kwa ajili ya Madaraja ya 1 na 2 ni kordi na maneno ya wimbo kwa ajili ya nyimbo zinazofaa kwa ajili ya kutumiwa na watoto. Kurekodi nyimbo katika lugha tofauti zinaweza kupakuliwa kwa kubonyeza hapa. Karatasi za kupaka rangikwa ajili ya masomo ya Daraja la 1 na mateuzi sambamba katika lugha tofauti zinawezakupakuliwa hapa.